Genesis 33:14-16

14 aHivyo bwana wangu umtangulie mtumishi wako, wakati mimi nikija polepole kwa mwendo wa makundi yaliyo mbele yangu na mwendo wa watoto, mpaka nifike kwa bwana wangu huko Seiri.”

15 bEsau akamwambia, “Basi na niwaache baadhi ya watu wangu pamoja nawe.”

Yakobo akauliza, “Lakini kwa nini ufanye hivyo, niache tu nipate kibali machoni pa bwana wangu.”

16 cHivyo siku hiyo Esau akashika njia akarudi Seiri.
Copyright information for SwhNEN